
Na Elizabeth John
BAADA ya kuwa kimya kwa muda mrefu, msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini, Best Nasso amesambaza kazi yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Tutoke’ hivi karibuni.
BAADA ya kuwa kimya kwa muda mrefu, msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini, Best Nasso amesambaza kazi yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Tutoke’ hivi karibuni.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Best Nasso alisema ngoma hiyo tayari imeanza kufanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio kutokana na mashairi yake kusimama.
“Naomba wapenzi wa kazi zangu wakae mkao wa kula kwaajili ya kuipokea video ya kazi hiyo ambayo naamini itafanya vizuri katika tasnia ya muziki huo kutokana na ukubwa wa mashairi ambayo yapo ndani yake,” alisema.
alisema mbali na hiyo kuna kazi nyingine amewaandalia mashabiki wake anaomba wasikae mbali na yeye ili wapate burudani iliyokamili.