Wazazi wa watoto waliozaliwa katika mkesha wa Sikukuu ya Krismasi katika hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam jana, wakiwa na afya nzuri pamoja na watoto wao. Kutoka kushoto ni Zamda Juma, Hadija Shaibu na Maria Joseph. (Picha na Francis Dande)
Muuguzi wa zamu katika hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam, Rashid Nyombiage akipima afya ya mtoto, Fredrick Mwita aliyezaliwa katika mkesha wa Sikukuu ya Krismasi.
Na Mwandishi Wetu
WATOTO 71 wamezaliwa wakati mkesha wa Krismasi katika Hospitali ya Amana na Temeke jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Tanzania Daima jijini, Muuguzi wa zamu katika Hospitali ya Amana Teresia Akida, alisema watoto waliozaliwa katika mkesha huo hospitalini hapo ni 52.wakiume ni 31 na wakike 21.
Akida alisema wazazi wa na watoto hao wanaendelea vizuri huku akidai mzazi mmoja alijuifungua mapacha watatu wakiume ambao siku zao zilikuwa hazijatimia.
Alisema changamoto kwa wazazi katika hospital hiyo ni vifaa vya tiba vinakuwa vinapungua hali inayosababisha kina mama kuagizwa baadhi ya vifaa vya kujifungulia.
“Mbali na changamoto hiyo pia tunakabiliwa na upungudfu wa watendaji katika hospitali yetu hivyo tunaomba serikali ilitupie jicho tatizo hilo”alisema.
Naye Muuguzi wa zamu katika Hospitali ya Temeke, Rashidi Nyombiage alisema watoto waliozaliwa katika mkesha huo hospitalin hapo ni 19 wakike tisa na wakiume 10.
Alisema waliozaliwa kwa njia ya upasuaji ni wawili lakini hali zao zinaendelea vizuri pamoja na wazazi wao.
Alisema changamoto inayokabili katika wodi za wazazi ni vitanda ni vichache havitoshelezi kwa kuwa kila siku wazazi wanaongezeka hali inayosababvisha walale wawili hadi watatu kwenye kitanda kimoja huku wengine wakilazimika kulala chini.
“Serikali ijaribu kutembelea hospital kuona changamoto na kuweza kujua jinsi gani ya kuzitatua”Alisisitiza Nyombiage.
Safi Mchala mkazi wa Tandika ambaye alijifungua katika hospital hiyo, alisema amefurahi sana kujifungua mtoto wa kike na kudai kuwa alikua anamuomba mungu ampe mtoto wa kike hivyo anamshukuru mungu kumpatia mtoto aliyemuomba.