Makamu wa kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad akimkabidhi Ngao ya Jamii nahodha wa timu ya KMKM, Khasim Ali baada ya kuifunga Shaba ya Pemba 2-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar juzi. Kulia ni Meneja Mauzo wa kinywaji cha Grandmalt, Kassiro Msangi. (Na Mpiga Picha Wetu)
Sehemu ya washabiki waliofurika kwenye Uwanja wa Amani mjini Zanzibar kushudia mchezo kati ya KMKM na Shaba kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii.