MITUMBWI mingi inayo timika katika kusafirisha abiria sehemu mbalimbali hapa nchini katika mito,maziwa na bahari imejengwa kwa njia za kienyeji na kwa kutumia mbao ambazo si elekeza kutoka mamlaka husika.
Kutokana na hali hiyo Mamlaka ya Udhibiti na usafirishaji nchi kavu na Majini (SUMATARA) imekusudia kutoa elimu kwa wanachi katika maeneo yanayo tumia usafiri wa maji kuacha kutumia mitimbwi ya kienyeji kwa ajili ya kusafirisha abiria kwenye bahari, maziwa na mito kutokana na vyombo hivyo kukosa ubora na umathubuti hali inayohatarisha usalama wa watu, vyombo na mali zao.
Akizungumza hivi karibuni katika maonyesho ya Sherehe za wakulima Nane Nane zinazo endelea kote nchini, kwa upande wa Nyanda za Juu Kusini zinafanyika katika viwanja vya John Mwakangale jiji Mbeya,Ofisa kutoka Mamlaka hiyo, Adam Mamilo, alisema mitumbwi mingi imejengwa kwa kienyeji tena kwa kutumia mbao ambazo si elekezi hivyo kukosa saifa za kuendelea kutoa huduma.
Mamilo alisema kuwa mitumbwi mingi inayo tumika katika maeneo mbaliumbali imejengwa kwa mbao ambazo hazikidhi viwango hali inayochangia kupoteza uhai wake ambao upo kwenye wastani wa miaka 3 hadi 5 ukilinganisha na miaka 35 kwa vyombo vilivyojengwa kwa viwango vya ubora.
Alisema kuwa hapa nchini mbao bado ina nafasi kubwa katika ujenzi wa mitumbwi hata hata kama bidhaa hiyo inapungua kila uchao na gharama zake zimekuwa zikiongezeka ikiwa ni pamoja na zile za ujenzi na kumba walio wengi wengi wana asili na ujuzi na kazi ya ujenzi wa Mitumbwi.
Alisema, kinachojitokeza katika hali hiyo,ni kupungua kwa ubora na umathubuti wa vyombo hivyo vinavyoundwa na kuhatarisha usalama wa watu, vyombo na mali.
Aliongeza kuwa kjutokana na hilo, mamlaka ilikichagua chuo cha Uvuvi Mbegani kufanya utafiti wa kina kuhusu ujenzi wa mitumbwi ya mbao inayotumika kusafirisha abiria na mali zao kwenye mito na maziwa.
Katika hatua nyingine Ofisa huyo aliwataka wananchi walio pata fursa ya kufika kwenye maonyesho yanayop en dlea kote kufika katika kwenye mabanda ya mamlaka hiyo ili kupata elimu juu ya kazi mbalimbali zinazo fanywa na mamlaka hiyo pia kutambua mbao zinazo faa kwa ajili ya kujengea mitumbwa ya kisasa.
Ofisa huyo alisema utafiti huo ulibaini kuwa miundo na uundaji wa boti au mitumbwi inayotumika hapa nchini ni ile ya kutumia miti mikubwa na kuchimba umbile la chombo na unatumika kwa vyombo vidogo kwenye baharini, maziwa na mtoni.