Quantcast
Channel: HABARI MSETO BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 19659

CEO NMB ASHIRIKI MKUTANO WA BENKI YA DUNIA ZANZIBAR

$
0
0


 Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Bi. Ruth Zaipuna akizungumza na Rais wa Benki ya Dunia, Ajaypal Singh Banga.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Bi. Ruth Zaipuna ameshiriki uzinduzi wa Mkutano Mkuu wa Benki ya Dunia (IDA20 Mid Term Review) unaofanyika kwa siku tatu Zanzibar.


Huu ni Mkutano wa 20, lengo likiwa ni kufanya tathmini ya Muda wa Kati kupitia Taasisi ya Kimataifa ya Maendeleo ya Benki ya Dunia.

Mkutano huo umefunguliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi - Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi na kuhudhuriwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar - Hemed Suleiman Abdalla, Waziri wa Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Mhe. Mwigulu Nchemba, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania - Emmanuel Tutuba na viongozi wengine.


Akiwa katika mkutano huo, Bi. Ruth alipata nafasi pia ya kukutana na Rais wa Benki ya Dunia - Ajaypal Singh Banga.

Benki ya NMB inajivunia kuwa sehemu ya kufanikisha mkutano huu mkubwa Tanzania unao wakutanisha wajumbe zaidi ya 3,000 kutoka mataifa takribani 100 duniani.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Hemed Suleiman Abdulla (kulia), akisalimiana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya NMB, Ruth Zaipuna (kushoto) wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa  20 wa Benki ya Dunia (IDA20 Mid Term Review), unaofanyika Zanzibar. (Na Mpiga Picha Wetu).
 

Viewing all articles
Browse latest Browse all 19659

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>