Mkurugenzi wa Kampuni ya ASET, ambao ni wamiliki wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’, AshaBaraka akiwashukuru wadau wa muziki waliohudhuria onesho maalumu kwa ajili ya siku ya Wanawake Duniani lililofanyika jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. (Picha na Francis Dande)
Baadhi ya wadau wa muziki wakicheza muziki wakati bendi ya Twanga pepeta ilipokuwa ikitumbuiza katika onesho maalumu kwa ajili ya kusherehekea Siku ya Wanawake Duniani lililofanyika katika Ukumbi wa Mango Garden jijini Dar es Salaam juzi.
Wadu wa muziki wakiwa katika onesho la bendi ya Twanga Pepeta wakati wa kusherehekea Siku ya Wanawake Duniani.
Mpiga tumba wa bendi ya Twanga Pepeta,Paul Philemon 'Kapashoo' akionesha umahiri wake.
Kiongozi wa bendi ya Twnga Pepeta, Lwiza Mbutu (kulia), akiwajibika jukwaani.
Mpenzi wa Twanga Pepeta akisakata muziki na Lwiza Mbutu.
Wanenguaji nao wakionesha manjonjo yao.
Wapenzi wa Twanga Pepeta wakiselebuka.
Lwiza Mbutu, Dogo Rama wakiwajibika.