Quantcast
Channel: HABARI MSETO BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 19659

Article 7

$
0
0
CHANNEL TEN SASA KUONEKANA DSTv
Na Janeth Jovin, TSJ

KAMPUNI ya Multichoice Africa na Afrika Media Group zimesaini mkataba wa kuonesha vipindi vya televisheni vinavyorushwa na Channel Ten.

 Mkataba huo utawafanya Watanzania wote nchini kupata nafasi ya kuona vipindi vya channel ten kupitia mfumo wa digitali wa DStv.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Afrika Media Group, Ramesh Patel alisema tunajivunia ushirikiano ambao tulikuwa tukiufanyia kazi kwa mda mrefu,nafasi hiyo ambayo imeletwa na huu mkataba utakuwa na faida kwa kampuni zote vilevile kwa watamazaji wetu, haswa katika kipindi hiki ambacho Tanzania imeama kutoka mfumo wa Analojia na kuingia katika mfumo wa digitali.

Chanel ten inaubora ambao unaendana na nchi yake ingali DStv inautaalamu wa tekinolojia hii itaongeza ubora wa kuwafikia watazamaji.

Akiongezea kuhusu DStv , Mkurungezi wa Multichoice Africa, East Afrika, Stephen Isaboke alisema Multichoice  inauwezo wa kuwaonyesha watu kwa masafa marefu na kwa upana zaidi kwa watazamaji wa ndani ya nchi. Ukiangalia ukuaji wa channel Ten tunaikaribisha kwenye ulimwegu wa DStv ambayo sasa imepanuka kwa channeli za Tanzania kufikia tatu ambazo ni TBc, Star Tv na sasa ni Channel ten.

Isaboke aliendelea  kusema  Tanzania itasonga mbele katika mfumo wa digitali, tungependa kuwahakikishia wapenzi  na wateja wetu kwamba DStv ilikuwa katika mfumo wa digitali zaidi ya miaka  17 .Kwa kupitia vifurushi mbalimbali tunawazawadi wateja wetu kuchagua vipindi mbalimbali vile wanavyovipenda.

Isaboke na Petal walimalizia kwa kusema kuwa watanzania watafurahia vipindi vya Channel Ten na vipindi vya kusisimua vilivyopo DStv.
 Meneja Uhusiano wa Multchoice, Barbara Kambogi (kushoto), Meneja wa vipindi wa Africa Media Group, Nicky Ngonyani (katikati) na Meneja Ufundi wa African Media Group, Augustino Mganga wakishika mikono kwa pamoja mara baada ya kusaini makubaliano yatakayowezesha vipindi vya televisheni ya Channel Ten kuonekana kupitia DStv. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam.
 Meneja wa vipindi wa Africa Media Group, Nicky Ngonyani (katikati) akizungumza na waandishi wa habari wakati walipoingia makubaliano ya kuonesha vipindi vya Channel Ten kupitia DSTv. 
 Meneja Ufundi wa African Media Group, Augustino Mganga akifafanua jambo wakati wa hafla hiyo.
 Meneja Uhusiano wa Multchoice, Barbara Kambogi (kushoto), akifafanua jambo wakati wa hafla hiyo.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 19659

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>