Quantcast
Channel: HABARI MSETO BLOG
Viewing all 19659 articles
Browse latest View live

NI VITA YA NDUGU CECAFA U-18 LNI VITA YA NDUGU CECAFA U-18 LEO, CHAMAZI COMPLEX

$
0
0


Na John Marwa


TIMU ya Taifa ya Tanzania ya wasichana (U-18) inashuka dimbani leo kuvaana na ndugu zao kutoka Visiwani Zanzibar  katika mashindano ya kuwania ubingwa wa ukanda wa Afrika  Mashariki na Kati  (CECAFA).


Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa majira y saa 12:00 ya jioni,  baada ya kukamilika kwa mchezo wa kwanza kati ya Ethiopia dhidi ya Burundi utakaopigwa saa 9:00 alasiri, ambapo michezo yote inalindima uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, Tanzania ikiwa mwenyeji wa mashindano hayo.


Tanzania inashuka dimbani wakitoka kupata matokeo mazuri katika michezo miwili ya awali waliyocheza kwa kuwafunga Burundi 3-0 na kushindi mabao 2-0 dhidi ya Ethiopia.


Wakati  Zanzibar, hii itakuwa mechi yao ya pili katika mashindano hayo baada ya kuanza vibaya kwa kukubalia kichapo cha mabao 3-0 dhidi ya Uganda. 


Katika mchezo wa leo timu zote zinahitaji matokeo kujiweka sehemu salama ya kuendelea na mashindano hayo huku Tanzania ikidhamilia kutwaa ubingwa wa CECAFA  U -18. Ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika mashindano hayo.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti makocha wa timu hizo, kocha wa Tanzania Bakari Shime alisema ni mechi ngumu, Zanzibar walionyesha kiwango kizuri katika mechi yao ya kwanza kwa kucheza vizuri kipindi cha kwanza dhidi ya Uganda.




“Hii mechi  sio rahisi, tunahitaji kupambana kushinda nina imani watakuja kivingine tofauti na walivyocheza mechi yao ya kwanza, kikubwa wachezaji wako tayari kwa ajili ya kupambana kusaka ushindi katika mechi yetu ya kesho (leo),” amesema Shime.


Amesema hakuna mechi rahisi,  haichukulii Zanzibar ni timu rahisi kwa sababu mechi ya kwanza walisumbuliwa na  Burundi na hatimaye kupata matokeo katika kupindi cha pili.


Naye  Kocha Mkuu wa Zanzibar,  Abdulmutik Haji amesema baada ya kufanyia kazi mapungufu ya mechi ya kwanza sasa wako tayari kusaka ushindi dhidi ya Tanzania.



“Tumejiandaa vizuri, wachezaji wangu wako tayari kwa mchezo huo, nina imani utakuwa mchezo mgumu na wenye ushindani kwa sababu tunahitaji kupata matokeo chanya dhidi ya Tanzania,” amesema Abdulmutik.


MWENYEKITI HALMASHAURI YA MJI KIBAHA AMUOMBA RAIS SAMIA KUPANDISHA HADHI KIBAHA KUWA MANISPAA

$
0
0

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha, Mussa Ndomba  akisoma waraka huo.
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha,Nickson Simon, akisalimiana na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Wilaya ya Kibaha (UWT) Mwalimu Mwajuma Nyamka wakati akiingia kwenye Ukumbi  wa Halmashauri ya Mji Kibaha.



Na Khadija Kalili, Kibaha

MWENYEKITI wa  Halmashauri  ya Mji Kibaha Mussa Ndomba  amemuomba  Mheshimiwa  Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan  kuipandisha hadhi Halmauri ya Mji Kibaha  na Kuwa Manispaa  kwa sawababu imekidhi sifa na vigezo kwa asilimia 78 kuwa Manispaa.

"Nasema haya kwa sababu Mkoa wa Pwani ni kati ya Mikoa mikongwe ambao umeasisiwa 1975 hivyo hata Halmashauri  ya Mji  Kibaha  ni Kongwe ambayo pia ni Makao Makuu ya Wilaya zote ndani ya Mkoa wa Pwani hivyo tunamuobma Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  atupandishe hadhi  na kuwa Manispaa  kwani jambo hili limeshazungumzwa sana  katika mikutano mbalimbali  ya Siasa  nchini kadhalika Mbunge wetu wa Jimbo la Kibaha Mjini Mheshimiwa Silyvestery  Koka amelisemea sana  akiwa katika vikao vya  Bunge Jijini Dodoma pia niwakumbushe ndugu wajumbe hata kwenye kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 jambo hili limezungumziwa kwenye majukwa ya siasa" amesema Ndomba.

Wakati huohuo Mwenyekiti  huyo amesema kuwa  kwa niaba ya Madiwani na  viongozi wa Halmashauri Kibaha anamuomba Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  kutoa idhini ya kumegewa eneo la Shirika la Elimu Kibaha kwa ukubwa wa ekari 576  lililopo kandokando ya  barabara  iendayo Morogoro  ikiwa ni katika  kuweka mandhari nzuri na ya kuvutia ya Halmashauri ya Mji  Kibaha iliyopo  Mkoani  Pwani kwa wanaoingia na kutoka.

"Mheshimiwa Rais  tunamuomba atupatie eneo la ukubwa  wa hekari 576 ili Halmashauri  iweze kuweka mipango miji mizuri ikiwemo uwekezaji kwa wafanyabiashara na kuuweka mji katika hali ya kuvutia pindi unapoingia, Kibaha ni  Wilaya mama na lango la kuingia Mji wa  mkubwa wa biashara Dar es  Salaam  tofauti na ilivyo hivi sasa  kwani  hakuna mandhari nzuri kwa sababu ya kuonekana mapori tu ambayo kwa sasa ni eneo linalomilikiwa na Shirika la  Elimu Kibaha  lenye ukubwa wa  hekari zaidi ya  3000 ambazo wahusika wameziacha zikiwa mapori   bila ya kufanya  jitihada zozote za kuendeleza katika eneo hilo"amesema Ndomba.

Amesema kuwa endapo Halmashauri  ya Mji Kibaha itapatiwa eneo hilo la ukubwa wa hekari 576 tu watapanga  shughuli  za  maendeleo  ya Mji Kibaha.

Mwenyekiti  Ndomba amesema hayo  katika kikao   cha Baraza la Madiwani cha robo ya nne ya mwaka  kilichofanyika mwishoni mwa wiki  na kuhudhuriwa na viongozi  mbalimbali  kutoka vya ma vya siasa , wakuu wa Idara zote  na wataalamu  ndani ya  Halmashauri  hiyo akiwamo Mkuu wa Wilaya Kibaha Nickson Simon, Mkurugenzi Mhandisi Mshamu Ali Munde pamoja  na   wananchi wa Wilayani hapa.

UTT AMIS yajivunia mafanikio

$
0
0

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya UTT AMIS, Simon Migangala, akizungumza na Wahariri wa Vyomba mbalimbali vya Habari kuhusu mafanikio ya utendaji kazi wa taasisi hiyo.

Mkuu wa Masoko na Uhusiano wa Kampuni ya UTT AMIS, Daudi Mbaga, akifafanua jambo wakati wa mkutano na wahariri wa vyombo mbalimbali vya habari uliofanyika jijini Dar es Salaam leo Julai 31, 2023 kuhusu mafanikio ya utendaji kazi wa  taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wahariri wakiwa katika mkutano huo.

Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Jukwaa la Wahariri (TEF), Angela Akilimali akitoa neno la shukrani wakati wa mkutano huo.

Benki ya NMB yadhamini Maonesho ya Nane Nane kwa Shilingi Mil. 80/-

$
0
0


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera (kulia) akipokea mfano wa hundi ya Shilingi milioni 80 kutoka kwa Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu - Frank Rutakwa kwa ajili ya udhamini wa Benki ya NMB katika maonesho ya Kilimo Nane Nane yanayofanyika Kitaifa Mkoani Mbeya.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Juma Homera (katikati) akifurahia pamoja na kamati ya maandalizi ya Maonesho ya Kilimo Nane Nane ya Mkoa wa Mbeya pamoja na Maafisa wa NMB, baada ya kupokea mfano wa hundi ya Shilingi milioni 80 kutoka kwa Kaimu Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu -  Frank Rutakwa (watatu kushoto) kama udhamini wa Benki ya NMB kwa maonesho hayo yanayoanza leo jijini Mbeya.


Na Mwandishi Wetu

 

Kwa kuthamini mchango wa kilimo katika ukuaji wa uchumi nchini, Benki ya NMB imedhamini Maonesho ya Nane Nane kwa kutoa shilingi milioni 80. Maonesho haya makubwa ya wakulima Nane Nane yanatarajiwa kuzikutanisha zaidi ya nchi 30 na kitaifa yanafanyika Jijini Mbeya kuanzia leo tarehe moja hadi tarehe Nane mwenzi huu.

 

Akikabidhi mfano wa hundi ya kiasi hicho cha fedha, kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Kaimu Meneja wa Kanda Nyanda za Juu - Frank Rutakwa amesema kwa kipindi cha miaka sita cha maonesho hayo ambayo yamekuwa yakifanyika Kitaifa mkoani Mbeya, Benki hiyo imedhamini jumla ya Shilingi Milioni 255.

 

Aliongeza kuwa, NMB imeweka idara maalumu ya Kilimo na Mameneja Uhusiano kwenye kila Kanda ili kuhakikisha kilimo kinafanikiwa na kinakuwa msingi imara kwa uchumi wa nchi yetu. Aidha, alisema kuwa ndani ya miaka minne, wamefungua zaidi ya akaunti 644,034 za wakulima nchi nzima. Mwaka huu kwa Mkoa wa Mbeya pekee, wamefanikiwa kufungua akaunti zaidi ya 87,044 za wakulima wa kahawa, mpunga, parachichi, mahindi nk.

 

Bw. Rutakwa alibainisha kuwa kupitia NMB Foundation, NMB imeweza kutoa elimu ya fedha na mfunzo ya biashara kwa vyama vya ushirika vya wakulima (AMCOS) 1,450 nchi nzima, ili kuwajengea uwezo wa namna bora ya kusimamia mapato yao. Huku kwa Nyanda za juu pekee wameshirikiana na AMCOs zaidi ya 555 zilizopo Mbozi (kahawa), Rukwa (Mahindi, Soya na Ufuta), Chunya  (Tobacco), Njombe (Viazi Ulaya)

Akizungumza mara baada ya kupokea mfano wa hundi ya shilingi milioni 80 kutoka Benki ya NMB, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya-Mhe. Juma Homera aliishukuru Benki ya NMB kwa msaada huo na kwa kuendelea kuwa karibu na wakulima kwa kuwasaidia pembejeo na Matrakta hivyo kusidia kukuza sekta ya kilimo nchini.

 

 “Benki ya NMB ni mojawapo ya taasisi za kifedha zinazoongoza nchini kwa kuchangia kwa dhati juhudi za serikali katika kukuza kilimo, ufugaji, uvuvi na sekta zingine hususani za Elimu na Afya ambazo wamekuwa mstari wa mbele kutoa michango mara kwa mara,” Alisema Mkuu huyo wa Mkoa.

 

 

Benki ya NMB yadhamini wafanyabiashara 10 kwenda Guangzhou, China kwa ziara ya siku tisa.

$
0
0

 

Mkuu wa Idara ya Biashara wa Benki ya NMB, Alex Mgeni (katikati) akimkabidhi mfano wa tiketi ya ndege Editha Kassim ambaye ni mmoja kati ya wafanyabiashara 10 wanaokwenda nchini China kwa ufadhili wa Benki ya NMB kwenda kutembelea Viwanda, Biashara na Masoko ya Kimataifa. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam Agosti 1, 2023. Kushoto ni Meneja Mwandamizi Idara ya Biashara NMB, Christopher Mgani. Hii ni mara ya Tatu Benki hiyo inawapa fursa wafanyabiashara kujifunza zaidi kutoka wenzao waliopo nchi za nje (Na Mpiga Picha Wetu).

 

Na Mwandishi Wetu


Benki ya NMB jana iliwaaga Wajasiriamali wadogo na wa kati 10 walioanza safari ya kujifunza ya siku tisa jijini Guangzhou, China kwa udhamini wa benki hiyo ilikijifunza mengi kutoka kwa taifa hilo ambalo limeendelea kibiashara.

Wafanyabiashara hao pamoja na mambo mengine wanatarajia kutembelea maonyesho ya biashara mbalimbali  kwaajili ya kujifunza masuala muhimu kwaajili ya biashara zao na pia kutembelea viwanda na masoko.

Akizungumza leo wakati wa hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Biashara NMB, Alex Mgeni, alisema safari hiyo ni utekelezaji wa mkakati wa benki hiyo unaolenga kuongeza thamani ya wateja wa benki hiyo huku akisisitiza kuwa safari hiyo itawapa washiriki mwanga mpya katika biashara zao.

“Kwa mara nyingine tena, benki ya NMB inawatangazia ya kuwa leo tuna kwenda kuwaaga wafanya biashara 10 ambao kwa udhamini wa benki ya NMB watasafiri kuelekea nchini China kwaajili ya kutembelea maonyesho ya biashara mbalimbali (Trade Fair) kwaajili ya  kujifunza masuala muhimu kwaajili ya biashara zao na pia kutembelea viwanda na masoko.

Tunatarajia leo (jana) mchana wataanza safari yao kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere kuelekea huko Guangzhou China, watapumzika Dubai na kuondoka kwenda Guangzhou. Watawasili Jumatano Majira ya saa nne usiku ya huko China. Hivyo wataanza rasmi Alhamisi ziara yao kwa kutembelea Mangesh ya biashara,” alisema Mgeni.

Mgeni alisema kuwa Benki ya NMB inaamini kuwa safari hiyo itakuwa na manufaa makubwa sana siyo tu kwa wafanyabiashara hawa lakini pia kwa taifa kwa ujumla. 

“Sisi kama benki ya NMB tunaamini kuwa ukuaji wa biashara zao utasaidia na kuchangia pato la taifa, kuongeza ajira, hivyo ni manufaa kwetu sote,”alisema.

Mgeni alisema kuwa benki yake imekuwa ikiwapeleka wafanyabiashara kipindi cha nyuma hata kabla ya janga la korona huku akibainisha kuwa waka jana, benki yake iliwapeleka wafanyabiashsra 10 nchini Uturuki. 

“Mwaka tunatarajia kupeleka jumla ya wafanya biashara 25.  Tunaanza na hawa 10. Mwezi wa Oktoba tunapeleka wengine 15 kwenye Maonyesho maarufu ya Canton Fair yanayofanyika huko huko China,” alisema.

Wakati wa hafla hiyo, Editha Kassimu mfanyabiashara kutoka mjini Tanga ambaye ni miongoni wa wafanyabishara waliopata fursa hiyo alishukuru benki ya NMB kwa kuchangia ukuaji wa biashara yake tangu mwaka 2011.
“Nilanza NMB mwaka 2012 baada ya kufungua akaunti kwa kiwango kidogo sana. Niliweza kukopa na kununua mashine ya ushonaji kwa shilingi laki moja na elfu 40. Najivunia kuwa na NMB kwa kuwa iliwezesha kuniwezesha na sasa hivi hivi namiliki mashine za kisasa zaidi ya 20 na natoa ajira kwa vijana wet,” alisema.

Aliongeza, “Katika safari hii ya China, natarajia kujifunza zaidi hasa teknolojia mpya na vitu vipya katika utendaji wa kazi yake,” 
Alisema baada ya kurudi nchini, anatarajia kutoa uzoefu atakaoupata kwa wafanyabiashara wenzake ambao hawajapta fursa hiyo huku akiishukuru benki hiyo kwa kuendelea kujitolea kuendeleza wafanyabiashara wadogo.

Mkuu wa Idara ya Biashara  wa Benki ya Alex Mgeni aliongeza kuwa benki hiyo imeshirikiana na Ubalozi wa Tanzania nchini China kufanikisha safari hiyo.

“Tumefurahi kuungana tena na wateja wetu siku ya leo na hii ni kuunga mkono falsafa yetu ya karibu yako. Leo ni mara ya tatu tangu tuanza zoezi kama hii. Wateja wengi ambao wanasafiri wanafanya biashara ya vifaa vya ujenzi, vipuli na biashara ya vipodozi,” alisema.
Aliongeza kuwa wateja hao watapata fursa ya kujifunza mengi kwa kuwa nchi ya China ni miongoni mwa nchi ambazo zimeendelea sana katika Nyanja hizo kwa kutumia teknolojia.

“Tunatarajia kuwa wafanyabiashara hawa watajifunza mbinu za kuzalisha kwa ubora na mafanikio zaidi na kuongeza tija katika biashara zao,” alisema.


KISA SIMBA DAY, WAUTAKA UWANJA WA UHURU

$
0
0

Na John Marwa

Uongozi wa Klabu ya Simba umeiandikia Serikali barua ya kuutaka Uwanja wa Uhuru kwa akili ya tamasha la wanasimba la Simba Day ''Unyama Mwingi' ambalo litafanyika Agosti 6 Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa klabu hiyo Murtanza Mangungu katika uzinduzi wa hamasa kuelekea kilele cha Simba Day.

“Tumeandika barua kuiomba serikali itupatie na Uwanja wa Uhuru kwa kuwa tunaamini tutaujaza Uwanja wa Mkapa mapema tu.”- Murtaza Mangungu, Mwenyekiti wa klabu ameongeza kuwa.

"Tukio hili la Simba Day wengine wameiga ingawa hawataki kukiri hilo. Wameondoa neno Day wameweka Wiki."-amesema.


UZINDUZI WA HAMASA NI UNYAMA MWINGI

$
0
0

Na John Marwa

Klabu ya Simba imezindua hamasa kuelekea kilele cha wiki ya Simba ambapo kitahitimishwa Agosti 6 Uwanja wa Benjamin Mkapa na siku ya wanasimba.


Simba Day Unyama Mwingi itafanyika Agosti 6 mwaka huu, ukiwa ni mwaka wa 14 wa tamasha hilo kubwa la michezo Barani Afrika ambalo hutumika kuwakutanisha wanasimba na kuwatambulisha wachezaji wao wa msimu mpya.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa hamasa uliofanyika Buza jijini Dar es Salaam kuelekea kilele cha Simba Day Meneja Habari na Mawasiliano wa Klabu hiyo Ahmed Ally amewataka wapenzi na mashabiki wa Simba kujitokeza kwa wingi kwani ndio utaratibu wao linapokuja jambo lao.

"Tumekuwa na utaratibu wa kupita eneo kwa eneo ili kuwafikia Wanasimba, kuwe kuna mabonde, milima ilimradi Wanasimba wenzetu wapo sisi tutafika ndio maana leo tupo hapa Buza. Lengo letu ni kuhakikisha tunawaalika Wanasimba mjitokeze kwa wingi kwa Mkapa siku ya Jumapili.”- Ahmed Ally ameongeza kuwa.

"Kuna mchezaji kila dirisha la usajili likifunguliwa wanamsajili lakini msimu ukianza anachezea Simba, njoo Jumapili kwa Mkapa mje mumwone." Amesema Ahmed.

Wapenzi mashabiki na wanachama wamejitokeza kwa wingi katika uzinduzi huo, jambo linalotoa ishara njema kuelekea kilele cha Simba Day.



WALIOSIMIKA MAWASILIANO YA INTANENTI KILELE CHA MLIMA KILIMANJARO WATUNUKIWA

$
0
0

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya  Habari, Mhe. Nape Moses Nnauye akikabidhi Tuzo na Vyeti kwa Wafanyakazi waliofanikisha ujenzi wa miundombinu ya mawasiliano ya intaneti na walioshiriki uzinduzi wa huduma ya Intaneti katika Kilele cha Mlima Kilimanjaro Disemba 13, 2023 katika hafla iliyofanyika Marangu Gate, mkoani Kilimanjaro.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya  Habari, Mhe. Nape Moses Nnauye akikabidhi Tuzo na Vyeti kwa Wafanyakazi waliofanikisha ujenzi wa miundombinu ya mawasiliano ya intaneti na walioshiriki uzinduzi wa huduma ya Intaneti katika Kilele cha Mlima Kilimanjaro Disemba 13, 2023 katika hafla iliyofanyika Marangu Gate, mkoani Kilimanjaro.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya  Habari, Mhe. Nape Moses Nnauye akikabidhi Tuzo na Vyeti kwa Wafanyakazi waliofanikisha ujenzi wa miundombinu ya mawasiliano ya intaneti na walioshiriki uzinduzi wa huduma ya Intaneti katika Kilele cha Mlima Kilimanjaro Disemba 13, 2023 katika hafla iliyofanyika Marangu Gate, mkoani Kilimanjaro.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya  Habari, Mhe. Nape Moses Nnauye akikabidhi Tuzo na Vyeti kwa Wafanyakazi waliofanikisha ujenzi wa miundombinu ya mawasiliano ya intaneti na walioshiriki uzinduzi wa huduma ya Intaneti katika Kilele cha Mlima Kilimanjaro Disemba 13, 2023 katika hafla iliyofanyika Marangu Gate, mkoani Kilimanjaro.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya  Habari, Mhe. Nape Moses Nnauye akikabidhi Tuzo na Vyeti kwa Wafanyakazi waliofanikisha ujenzi wa miundombinu ya mawasiliano ya intaneti na walioshiriki uzinduzi wa huduma ya Intaneti katika Kilele cha Mlima Kilimanjaro Disemba 13, 2023 katika hafla iliyofanyika Marangu Gate, mkoani Kilimanjaro.

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya  Habari, Mhe. Nape Moses Nnauye akikabidhi Tuzo na Vyeti kwa Wafanyakazi waliofanikisha ujenzi wa miundombinu ya mawasiliano ya intaneti na walioshiriki uzinduzi wa huduma ya Intaneti katika Kilele cha Mlima Kilimanjaro Disemba 13, 2023 katika hafla iliyofanyika Marangu Gate, mkoani Kilimanjaro.

WAZIRI wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (Mb) amekabidhi tuzo na vyeti kwa Wafanyakazi na wadau walioshiriki katika zoezi la kufanikisha mradi wa usimikaji wa huduma ya Intaneti katika Mlima Kilimanjaro.

Akikabidhi tuzo hizo, Mhe. Nnauye alisema mafanikio ya kuimarisha Mawasiliano ya Intaneti katika Mlima Kilimanjario ni kielelezo tosha kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kukuza matumizi ya TEHAMA na kukuza sekta hii ya Mawasiliano ambayo ni ingini ya ujenzi wa uchumi. 

Alisema kufanikisha kwa mradi huo wa mawasiliano kunaenda kuongeza thamani Mlima Kilimanjaro sambamba na kuimarisha sekta ya Utalii nchini ukizingatia kuwa Idadi ya Watalii wanaotembelea nchi yetu imezidi kuongezeka.

"..Hivi sasa tumeanza kuona matukio yakifanyika katika Mlima Kilimanjaro, SIMBA sports Club jana tarehe 21/07/2023 imezindua jezi zake katika kilele cha Mlima Kilimanjaro, Mpiga Kinubi maarufu Duniani, Siobhan Brady ni Mwanamuziki na Mpiga Kinubi aliyeshinda tuzo za Guinness kwa kupiga Kinubi katika Milima ya Himalaya, yupo Tanzania na anatarajia kupiga Kinubi akiwa katika kilele cha Mlima Kilimanjaro, ni matumaini yangu kuwa uwepo wa intaneti kutasaidia kutangaza tukio hilo sambamba na kuutanga mlima wetu.

Aidha aliongeza kuwa, zipo faida lukuki za uwepo wa mawasiliano ya Intaneti katika Mlima Kilimanjaro zikiwemo kukuza sekta ya utalii, kutengeneza mazingira rafiki kwa watalii kupata huduma za mawasiliano pamoja na watoa huduma za kitalii, TTCL kujipatia mapato kutoka kwa watumiaji huduma hizo, Serikali kupata mapato, sambamba na kuimarisha Ulinzi na usalama eneo la Hifadhi. Mradi pia utasaidia Serikali kupitia Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari katika utekelezaji wa  mkakati wa kujenga Tanzania ya Kidijitali.

Awali akizungumza katika hotuba yake, Mkurugenzi Mkuuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania, Eng. Peter Ulanga alibainisha kuwa Shirika la Mawasiliano Tanzania litaendelea kuhakikisha huduma ya Intaneti inapatikana muda wote na yenye kasi kwa wateja wetu ili kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita(6) inayoongozwa na Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kutangaza vivutio vya Utalii nchini. 

"Tangu huduma hii izinduliwe huduma ya Intaneti katika kilele cha Mlima Kilimanjaro, ambayo imenufaisha Watalii na wasio watalii, jumla ya zaidi ya watumiaji 24,837 wametumia huduma hiyo tangu tuanze mradi mwezi wa Agosti mwaka jana 2022 na tunatarajia kuwa katika kipindi cha msimu wa Watalii ambao umeanza sasa idadi ya watumiaji itaongezeka. Kuongezeka kwa watumiaji kutasaidia kuongezeka kwa mapato ya Shirika na nchi kwa ujumla". Alisema Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, Eng. Ulanga.

Akifafanua zaidi juu ya mradi huo, Eng. Ulanga alibainisha ujenzi wa mradi huo ni kazi nzuri iliyofanywa na Wahandisi wazawa wa TTCL hivyo wana kila sababu ya kuwapongeza kwa kazi ya kizalendo waliyoifanya licha ya mazingira ya utekelezaji wa kazi hiyo kuwa magumu sana. Alitumia nafasi hiyo kuwashukuru 'Porters' zaidi ya 200 waliofanya kazi ya kubeba vifaa vya mawasiliano na kupandisha katika maeneo ambayo ujenzi ulikuwa ukifanyika. 

"...Hii inaonesha jinsi gani tumepiga hatua kama Taifa yakuwa na wataalam wa kuweza kufanya kazi hizi bila kuhitaji msaada wa wataalamu kutoka nje ya nchi. Kwa mara nyingine naomba ninawashukuru na kuwapongeza kwa weledi waliouonesha katika kukamilisha mradi huu kwa wakati." Alisisitiza, Eng. Ulanga katika hotuba yake.

Hata hivyo, ili kuongeza wigo wa upatikanaji wa huduma ya mawasiliano ya Intaneti kwenye vivutio vya Utalii nchini, TTCL imeanza ujenzi wa Mkongo wa Mawasiliano katika njia ya Machame Gate na inatarajia kukamilisha mradi huo kabla ya mwezi Septemba mwaka huu 2023. Aidha, mradi wa kupeleka Intaneti kwa njia ya Wi-Fi kwenye maeneo ya umma (Public Wi Fi), umeanza katika Vyuo Vikuu, ikiwemo ufungaji wa 'Wi-Fi' katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam katika College of Information and Communication Technologies (CoICT). Na vyuo vingine ambavyo viko katika hatua za awali za utekelezaji mradi.

"Katika utekelezaji wa Mkakati wa Shirika, hivi sasa tunatekeleza mradi wa FAIBA MLANGONI KWAKO ambapo tunapeleka huduma ya Intaneti kwenye makazi na ofisi. Huduma hii ni BURE, mteja ataingia gharama ya kununua Kifurushi tu ambacho gharama yake inaanzia shilingi Elfu Hamsini na Tano (55,000/-). Huduma hii itasaidia pia kupunguza gharama za bando kwa Wananchi wetu," alieleza Eng. Ulanga.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Mawasiliano - TTCL Tanzania, Bi. Zuhura Sinare Muro akizungumza katika hafla hiyo, alisema Bodi ya Wakurugenzi inafarijika kuona matukio makubwa yameanza kuonekana mubashara kwenye Mlima Kilimanjaro, mbali na Serikali kupata mapato jambo ambalo linaendelea kuvitangaza vivutio vya taifa Kitaifa na Kimataifa.

Jumla ya Wafanyakazi 14 waliofanikisha zoezi hilo walikabidhiwa vyeti na tuzo wa wakiwemo wafanyakazi 11 wa TTCL na wafanyakazi watatu wa KINAPA, pamoja na makundi mengine yalioshiriki ufanikishaji zoezi zima.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Mawasiliano - TTCL Tanzania, Bi. Zuhura Sinare Muro (wa pili kulia) akisalimiana na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye (Mb) mara baada ya kuwasili kwenye hafla ya kuwatunuku tuzo na vyeti Wafanyakazi na wadau walioshiriki katika zoezi la kufanikisha mradi wa usimikaji wa huduma ya Intaneti katika Mlima Kilimanjaro. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mkuuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania, Eng. Peter Ulanga akifuatilia.



UWANJA WA AMAAN ZANZIBAR WAKAGULIWA MAANDALIZI YA AFCON 2027

$
0
0

Na Eleuteri Mangi, WUSM, Zanzibar

Timu ya Wakaguzi ya utayari wa nchi za Kenya Uganda na Tanzania kuhusu utayari wao wa kuwa wenyeji AFCON 2027, leo hii Julai 31, 2023 wapo Zanzibar ambapo wamekagua Uwanja wa Amaan, hospitali ya Mnazi Moja, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Aman Karume pamoja na viwanja vingine vya mazoezi.

Timu hiyo kutoka Shirikisho la Mpira Afrika (CAF) imezungukia maeneo hayo ikiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania Bw. Wallace Karia na Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar Bw Suleiman Mahamud Jabir.

Maafisa wengine kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakiwemo Kaimu Mkurugenzi wa Michezo Bw. Ally Mayayi na Katibu Mtendaji Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Bi. Neema Msitha na kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ni Kamishna Idara ya Michezo Bw, Ameir Mohammed, Katibu Mtendaji Baraza la Michezo Zanzibar Saidi Marine pamoja na maafisa wengine kutoka TFF na ZFF.


UTT AMIS yaita wananchi kuwekeza kisasa zaidi

$
0
0


*Yageuka kimbilio kwa wenye vipato tofauti, faida sasa Trilioni 1.5/-

Na Beatrice Sanga-MAELEZO

KAMPUNI ya Uwekezaji wa Mitaji ya Pamoja (UTT AMIS) imetoa rai kwa wananchi kuwekeza kwenye mifumo mbalimbali ya kampuni hiyo ili kuweza kujikimu  kimaisha na kuwa na uhakika wa maisha ya sasa na ya baadae ambapo kwa sasa inaendelea kuelimisha wananchi kuhusu  uwekezaji huo na kwamba imekuwa kimbilio la wengi bila kujali vipato vyao.

Hayo yamebainishwa Julai 31, 2023 Jijini Dar es Salaam wakati wa Mkutano wa Msajili wa Hazina, UTT AMIS, Wahariri na waandishi wa habari wenye malengo ya kuelezea majukumu na namna gani kampuni hiyo inafanya kazi.


Mkurugenzi Mtendaji wa UTT AMIS, Simon Migangala amebainisha kuwa majukumu yao ni kuboresha  huduma  na faida  kwa wawekezaji  wadogo na wakubwa wa Kampuni hiyo ili kuvutia uwekezaji.

"UTT tunakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo watu wengi kukosa uelewa na elimu ya masoko ya fedha pia watu wengi hawana kipato kikubwa cha kuwekeza tumezingatia shida zetu kuliko kuwekeza tunahitaji kuwekeza kwa malengo ya baadae," amesema Migangala.

Aidha, Migangala amebainisha kuwa huo ni mwendelezo wa uelimishaji kuhusu majukumu yanayofanywa na Kampuni hiyo ili kuhakikisha elimu inawafikia wananchi wote bila kuangalia kipato chao.

Amesema mifuko ya UTT AMIS imeboreshwa kwa  uwekezaji wenye malengo ya muda mrefu na muda mfupi ili kuhakikisha kila mtanzania anawekeza kwa maslahi yake na taifa kwa ujumla.

"Maisha yetu Tunategemea fedha, ikiwa tofauti na miaka ya zamani kwa wengi tulikuwa tunarithishwa ardhi, lakini sasa hivi urithi wetu unategemea kwenye uwekezaji wa fedha hivyo niwahimize kuwekeza UTT AMIS, kwani kila mtanzania atajivunia," amesema Migangala.

Akizungumzia mafanikio ya miaka minne mfululizo waliyopata kutokana na uwekezaji mdogo na mkubwa, Mkurugenzi huyo amesema kuwa Kampuni hiyo imeweza kuchangia katika Pato la Taifa na kutoa gawio kwa kila mwaka kupitia ofisi ya Msajili wa Hazina.

"Mafanikio  haya ni kwa mwaka juzi 2021 ukuaji wa Taasisi  kutoka bilioni 600 hadi bilioni 996 sawa na asilimia 50 kwa mwaka  2022 kutoka bilioni 996 hadi trilioni 1. 5 sawa  na asilimia 54 ukuaji huu umeenda  vizuri  ikiwa ni tofauti na miaka ya nyuma," amefafanua Migangala

Amesema  kwa  mwaka  wa fedha  2023/2024 ambao ulianza Julai mwaka huu  ukuaji  umeongezeka hadi kufikia asilimia 12 na kuweza kuchangia kwenye pato la Taifa kwa miaka sita mfululizo.
Aidha, amewataka  Watanzania  kuendelea kuwekeza  kwa sababu   Kampuni hiyo  iko imara kwani kuwekeza ni fursa kwa mwekezaji  mdogo na mkubwa  wanapata faida sawa.

Kwa upande wake Angela Akilimali ambaye ni Mjumbe Jukwaa la Wahariri nchini (TEF) amesema kuwa UTT AMIS inatakiwa kuendelea kuelimisha jamii kuhakikisha kuwa wananchi wanachangamkia fursa ya uwekezaji katika mfuko huo.

“Timu hii iko imara inawakilisha waandishi wengine ambao hawajafika hapa na tutahakikisha ujumbe wenu unafika na watu wanaitambua UTT AMIS, Taasisi ambayo ni nzuri ya uwekezaji lakini wengine wanashindwa kufahamu, nina imani hii elimu ambayo tumeipata hapa imetufafanulia zaidi kwamba hata mtu wa hali ya chini anaweza kuwekeza katika masuala ya UTT AMIS, huko mtaani watu wana mawazo mengi, wanakuwa hawaelewi wapi waende ili kuwekeza kwa ajili ya watoto wao.” Amesema Akilimali.

Ofisi ya Msajili wa Hazina imeendelea na utaratibu wake wa kukutanisha Taasisi mbalimbali zilizopo chini ya ofisi hiyo na Wahariri wa vyombo vya habari pamoja na waandishi ambapo leo Kampuni ya UTTM AMIS imepata nafasi na kuzungumzai mafanikio yao na mwelekeo wao.

MIZENGO PINDA AFUNGUA MAFUNZO YA VIONGOZI SHULE YA UONGOZI YA MWALIMU NYERERE

$
0
0


 Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda akizungumza kwenye ufunguzi wamafunzo ya Uongozi  kwa viongozi  leo Julai 31  kwenye Shule  ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo  maeneo ya ya Kwamfipa wilayani Kibaha mkoani Pwani.

 

Na Khadija Kalili

WAZIRI Mkuu Mstaafu wa awamu ya tatu  Mheshimiwa Mizengo Kayanza  Peter  Pinda  leo amefungua mafunzo kwa Viongozi  kutoka katika Taasisi mbalimbali  za seeikali  mafunzo hayo ya Uongozi na Maadili yanayofanyika kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere iliyopo Wilayani Kibaha Mkoani Pwani.

Akifungua mafunzo hayo leo Julai 31  wa  Chama na Serikali  kujiendeleza  na elimu ya Uongozi ili waweze kuwasimamia vyema wanaowaongoza  katika sehemu zao za  kazi  huku amesema kuwa    kwamba elimu haina mwisho.


Amesema kuwa upo umuhimu wa  akitoa wito wa kuwaendeleza wataalamu  mbalimbali  kwa lengo la kuwajengea uwezo ,uzalendo wa nchi yao jambo ambalo litachochea wqtu kufanya kazi kwa bidii, juhudi,maarifa makubwa na kutojali kuona wanapoteza nguvu zao kwa kiasi gani.

 "Uzalendo ni dhana yenye wigo mpana zaidi hivyo jambo hili ni la muhimu mtu kukaa darasani na kupikwa ili pindi anapomaliza mafunzo haya atoka akiwa  ameiva  na kuelewa dhana halisi ya kua mzalendo ndani ya nchi yako, zamani viongozi  walipikwa pindi walipoteuliwa tofauti na ilivyo sasa hivyo ili  kuongeza ufanisi katika uongozi  nashauri viongozi wakiwemo Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na watu wa kada mbalimbali  wawekewe utaratibu  wa kupata mafunzo kama haya mara kwa mara"amesema Mheshimiwa  Pinda.

Akifungua mafunzo hayo ya wiki moja Mheshimiwa  Pinda amesema kuwa amefurahishwa kuona uwiano wa washiriki wa mafunzo hayo ambapo jinsia zote zimeshirikiswa ipasavyo.

Amesema kuwa wakati umefika wa  kuwajengea uzalendo wananchi wa kada zote wakiwamo wanafunzi  huku akitolea mfano wa nchi ya Izrael namna ambavyo wamewajengea  wananchi wao kuipenda na kuithamini nchi yao huku akisema kuwa kila Mtanzania  anapaswa kuwa mzalendo licha ya kuwa na itikadi tofauti za kidini, kabila  na rangi lakini wote wawe  kitu kimoja.

Ametoa sifa kwa uongozi  wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere  kuwa licha ya kuwa hakina muda mrefu lakini matunda yake yameanza kuonekana na maua yake yamechanua kutokana na mafunzo waliyopatiwa watu  mbalimbali wakiwemo wanasiasa , viongozi wa  ndani na nje ya nchi.

"Viongozi  wangu katika serikali naomba tuwajibike kikamilifu, kwanza wajibika halafu dai haki yako  kila Kiongozi  anapaswa kuwa mbunifu na mzalendo katika Taasisi yake na  kuwajibika ipasavyo.

"Mashirika makubwa na Taasisi nyingi za serikali  zinayumba sababu Viongozi  wengi siyo waadilifu,kitu kinachoitwa uadilifu ni kigumu lakini endapo utakaa na kina babu ambao ni wakongwe  kuna mambo  mazuri  unaweza kuyapata  binafsi naweza sema nimepata bahati ya kufanya kazi  na viongozi   wakongwe  wengi ambao ndiyo walionijenga  natumia mfano huu ikiwa ni lengo la kutaka kuwakumbusha  umuhimu wa kuthamini wazee katika utendaji  wetu" amesema Pinda.

"Nasisitiza uadilifu na kuacha maovu ambayo yanaathiri jamii kwa ujumla ndiyo maana CAG akitoa ripoti  yake inakua imejaa madudu mengi yote haya ni  kutokana na upungufu wa maadili  ya uongozi kwa baadhi ya viongozi  nchini ". amesema  Waziri Mkuu Mstaafu wa awamu ya tatu Mheshimiwa  Pinda.

Ametoa rai  kwa uongozi  wa Shule ya Mwalimu Nyerere kuwepo na utaratibu wa kutoa mafunzo  mafupi yanayohusu uongozi, uzalendo  na  uendeshaji nchi kwa ujumla .

"Wateule  wote wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) jipangeni ili mje kupata mafunzo hapa itumieni  fursa ya Shule hii ya siasa kuwapika makada wa chama ili waweze kukinadi chama kwa weledi wa hali ya juu"amesema.

Mkuu wa Shule hiyo ya Mwalimu Nyerere Prof.Marceline Chijoliga  amesema kuwa  wanajivunia kwa kutoa mafunzo bora  kwani hadi sasa  tayari zaidi ya wahitimu 2,000 wamepata mafunzo katika  Shule hiyo.

"Mapema mwezi huu jumla ya viongozi  wanawake 71 wamehitimu mafunzo  yaliyowashirikisha  washiriki kutoka katika Taasisi mbalimbali  nchini  na wamehitimu vyema hivyo tunatarajia watakua viongozi bora huko waliko,  mafunzo waliyopata  yamewajengea uwezo viongozi hao wanawake  na ambao wanauzoefu  siyo chini ya miaka mitano ambayo yamefanyika kwa mara yakwanza hapa nchini  ambapo wahitimu wamefundishwa  mbinu bora  za Uongozi  wa Utawala  Bora  katika Taasisi wanazoziongoza.


Aidha ufunguzi huo umehudhuriwa na viongozi wa chama na serikali akiwamo Mheshimiwa  Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Simon , Mwanasiasa Mkongwe  nchini  ambaye ameshika nyadhifa mbalimbali  Mzee Paul Kimiti.

Mstaafu Paul Kimiti amewahimiza  viongozi hao kuwa wazalendo ndani ya nchi yao.

Amesema kuwa hakuna aliye  juu zaidi ya mwingine hivyo amesisitiza kuwa kila mmoja anamtegemea mwenzake  na kusema kuwa katika maisha epuka  kufanya  maamuzi katika jambo lolote  bila kushirikisha  wenzako wengine wanao kuzunguka kwani  hiyo  ndiyo sifa ya Kiongozi  bora.

"Kiongozi bora huheshimu   anaowaongoza na kuwashirikisha   bila ya kujali umri ,itikadi zao za  dini na mambo mengineyo yanayowatofautisha.
 

Waziri Makamba azindua Mpango Mkakati wa TANESCO wa Miaka 10

$
0
0
Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam

Waziri wa Nishati January Makamba amezindua Taarifa ya Mwaka wa Fedha 2021/2022 na Mpango Mkakati wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wa Miaka 10.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo uliofanyika leo jijini humo, Waziri Makamba amelipongeza TANESCO kwa hatua nzuri kuelekea mabadiliko makubwa ya Shirika ambayo hayajapata kutokea.


“Hii haijapata kutokea, sisi tunachoomba kwa wananchi, wadau na wateja Wetu ni kuwa na subira, kwani mabadiliko yanahitaji muda mrefu,” amesema Waziri Makamba na kuongeza,

“Mabadiliko yanayofanyika TANESCO yanaweza yasieleweke haraka,”.


Waziri Makamba amebainisha kuwa kama Serikali wataendelea kuliunga mkono shirikisho hilo ili kufikia malengo na mipango ya TANESCO.


Hivyo amesema kwamba Serikali inafanya juhudi ya kuitafimutia Mtaji wa kutosha ili kufikia malengo yake.


Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Maharage Chande, akieleza kuhusu mafanikio kwa Mwaka wa Fedha 2021/2023, amesema kwamba Shirika limeweza kupata faida ya Sh Bilioni 109.


Kadhalika wameweza kuanzisha namba moja ya huduma kwa wateja, kuunganisha wateja 504,366, kupungua kwa upotevu wa Umeme kutoka asilimia 14.5 hadi asilimia 15 lengo lililowekwa.


Kwamba wanaendelea kuitekeleza Miradi ya kimkakati ukiwemo Mradi wa Mwalimu Julius Nyerere ambao umefikia asilimia 90.


Akizungumzia kuhusu Mpango mkakati wa miaka 10 ijayo, Chande amesema wamejipanga kuwekeza kufanyakazi kidigitali, kuongeza juhudi za kutatua changamoto za wananchi na kuhakikisha kuna mtiririko mzuri wa kifedha.

Nae, Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO, Omary Issa ameeleza kuwa Shirika linamkakati mkubwa wa kuandaa Vijana watakao kuja kuliendesha kwa miaka ijayo.


Hivyo amesema kwa sasa kuna kikundi cha watu kiko nje ya Nchi kikipata mafunzo na kwamba hawataishia kwa kikundi hicho tu bali wataendelea na kwa wengine.


 

Azam TV yazindua Tamthiliya Mpya Mbili, yawataka Watazamaji wake kukaa tayari kuzipokea

$
0
0
Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam

Azam TV kupitia Chaneli yake ya Sinema Zetu imezindua tamthilia mbili za moto, ambazo ni “Mtaa wa Kazamoyo” na “Lolita” na zitaanza kuonyeshwa kwenye chaneli ya Sinema Zetu kuanzia tarehe 4 na 14, Agosti 2023 katika Chaneli ya Sinema Zetu namba 103.

Akizungumza na wanahabari Jijini humo Mkuu wa Chaneli ya Sinema zetu Sophia Mgaza amesema katika kutimiza msemo wao maarufu wa ‘burudani kwa wote’, Azam TV vinara wa huduma bora za maudhui na burudani za kusisimua nchini, kwa mara nyingine tena wanajivunia kutangaza uzinduzi wa tamthilia hizo zilizokuwa zikisubiriwa kwa muda mrefu.


 

Amebainisha kuwa tamthilia hizo zilizobeba simulizi za kuvutia si tu kwamba zinakuja kuleta mapinduzi ya tasnia ya tamthilia nchini, bali zinaakisi maisha halisi ya Watanzania wa rika zote na zinahusisha waigizaji wenye vipaji na viwango vya juu.

“Uzalishaji wa tamthilia hizi mbili Mtaa wa Kazamoyo na Lolita umezingatia mahitaji ya soko kwani umetumia vifaa vya uzalishaji vya kisasa na ubora wa hali ya juu wenye uwezo wa kutoa kazi katika viwango vya picha zenye ubora na angavu yaani HD (High Definition). Lengo letu la kufanya mambo yote haya ni kuendeleza dhamira yetu ya kutoa burudani ya hali ya juu kwa watazamaji wetu”Amesema  Sophia Mgaza.

Amesisitiza kuwa Mtaa wa Kazamoyo na Lolita zimesanifiwa kwa uangalifu mkubwa ili kuwapa watazamaji aina mbalimbali za simulizi za hadithi zenye kulinda maadili ya Kitanzania, kutoa elimu kwa jamii na zinazotazamika na familia yote na kutimiza majukumu yote matatu ya msingi yaani kuhabarisha, kuburudisha na kuelimisha jamii.

Tamthiliya ya Mtaa wa Kazamoyo na Lolita zimetayarishwa kwa ustadi mkubwa zikishirikisha waigizaji mahiri, waandishi wenye ujuzi na watayarishaji wazoefu na zinajumuisha viwango vya juu vya uzalishaji na mbinu za hali ya juu ili kuhakikisha utazamaji wa kuvutia kwa hadhira.

Ameongeza kuwa waanatarajia kuanza kupokea filamu hivi karibuni ambazo wanategemea kupata hadithi zenye utafiti wakutosha, uhalisia wa kitanzania na kugusa jamii ya kimataifa na hadithi zenye stori ndefu isiyopungua dakika 90 na yenye viwango vya juu vya kimataifa inayoweza kuchezwa kwenye majumba ya Sinema pamoja na bajeti yake.

Kwa upande wake, Muandaaji wa  Tamthilia ya Mtaa wa Kazamoyo, Mahsein Awadhi (Dkt. Cheni) amesema tamthilia hiyo inasimulia hadithi inayohusu maisha ya uswahilini na matukio wanayopitia wakazi wa Mtaa wa Kazamoyo. Huu ni mtaa wenye sifa ya wanawake kukaa vibarazani na kupiga stori, porojo pamoja na umbea huku vijana wa mtaa huu wakichagua maisha ya kuwa vibaka ili kupata vipato kwa njia fupi na nyepesi kwao.

Katika Mtaa huu viongozi wa Serikali ya Mtaa wanashindwa kudhibiti vitendo hivyo na unaweza kusema wanafurahishwa na tabia za wakazi wake na ndio maana wanakuwa mstari wa mbele kutetea maovu yanayoendelea dhidi ya vyombo vya dola.

Katika Mtaa wa Kazamoyo si ajabu kukuta watu wazima wakijihusisha kimapenzi na vijana wadogo. Hii ni hadithi iliyojaa msisimko, migogoro na hadithi za kuvutia kuhusu maisha halisi ya uswahilini.

“Tamthilia hii imezalishwa na Kampuni ya Cheni Arts Creation Company Limited na baadhi ya wasanii mashuhuri walioshiriki katika tamthilia hii ni pamoja na Mahsein Awadhi (Dkt. Cheni), Amina Ahmed, Mwene Shina, Ester Darwesh, Elizabeth Chijumba, Queen Masanja, Hashim Kambi, Abdallah Mkumbila (Mzee Muhogo Mchungu), Pili Lway (Mama Nyamayao) Hajji Seif, Amini Samofi, Karim Mandonga na wasanii wengine wengi waliopo katika tasnia na wale wanaochipukia.” Amesema Dkt.Cheni.

Nae, Muandaaji wa Tamthilia ya Lolita, William Mtitu amesema tamthilia hiyo inatoa simulizi ya maisha ya vijana wa kisasa na namna wanavyokabiliana na changamoto za kimahusiano yaliyojaa usaliti. Tamthilia hii pia inatoa simulizi ya familia mbili zilizodhulumiana pesa na hivyo kila upande ukiapa kulipiza kisasi kwa mwenzake, lakini kabla kisasi hakijakamilika familia mojawapo inapata ajali ya ndege na kufariki dunia na hivyo kumwacha binti yao kipenzi katika malezi ya familia hasimu ya wazazi wake.

Familia hiyo inaamua kudhulumu mali zote zilizoachwa na wazazi wa binti huyu ambaye baadaye anakuja kupendana na mtoto wa kiume wa familia hii na siku ya harusi yao anapata ajali mbaya ya gari na hivyo kumsababishia ulemavu.

Ajali hiyo imesababishwa na kijana aliyekuja kugundulika baadaye kuwa ni ndugu yake wa damu. Baada ya ajali hii, siri nyingi zinaanza kugundulika kuwa rafiki yake kipenzi ana uhusiano wa kimapenzi na mume wake, huku mume wake naye akiwa na mpango wa kumdhulumu mali zote alizoachiwa na baba yake. Kugundulika kwa siri hizi kunazua migogoro na hali ya sintofahamu katika jamii inayowazunguka. Tamthilia hii imejengwa na migogoro mingi ya kimapenzi baina ya marafiki, wazazi na vijana wadogo na kati ya familia na familia. Ni simulizi ambayo unatakiwa kuiona mwenyewe ili kuielewa vizuri.

“Tamthilia hii imeandaliwa na Magazijuto Pictures chini ya muandaaji William Mtitu. Miongoni mwa waigizaji mashuhuri katika tamthilia hii ni pamoja na Angel Mazanda, Mariam Ismail, Christopher Mziwanda, Romeo George, Genevieve Mpangala, Dennis David, Gysell Ngowi, Sadam Nawanda, Cojack Chilo, Careen Simba, Jacqueline Materu, Neema Malita, Khalid Kuraish na wasanii wengine wengi wanaofanya vizuri katika tasnia ya filamu Tanzania” Amesema Bw. Mtitu.

Hata hivyo tamthilia hizo zinachukua nafasi ya Fungu Langu itakayofikia tamati tarehe 29 Julai 2023 na Jeraha itakayofikia tamati tarehe 10 Agosti, 2023 ambapo Burudani zote hizo zinapatikana kwa malipo ya kifurushi cha Shilingi 8,000 kwa watumiaji wa kisimbuzi cha dishi na antena.

KAMPUNI YA ASAS YAPONGEZWA

$
0
0

Mkuu wa wilaya Mufindi, Dk. Linda Salekwa akikabidhi Kajuna Maurice zawadi ya bingwa wa mashindano ya gofu ya wazi ya Mufindi 2023

 

NA DENIS  MLOWE, MUFINDI


MKUU wa wilaya ya Mufindi Dr.Linda Salekwa  ametoa pongezi kwa kampuni ya Asas wazalishaji wa maziwa Bora nchini ya Asas kwa kudhamini mashindano ya mchezo wa Gofu ya Mufindi Southern Open Championship 2023 na kushudia Kajuna Maurice kutoka Lugalo gofu akiibuka bingwa wa mashindano hayo.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi zawadi kwa bingwa na washindi mbalimbali wakiwemo wanawake na wazee wenye umri wa zaidi ya  miaka 60 na kuendelea , Dr. Salekwa alisema kuwa kampuni ya Asas imekuwa faraja kwa jamii ya wanamichezo hivyo lazima waungwe mkono ili kuendelea kujitoa katika kudhamini michezo mbalimbali nchini.


Licha ya kuipongeza kampuni ya Asas alitoa wito kwa Wanawake wajitokeze kwa wingi kushiriki michezo mbalimbali hususani mchezo wa Gofu kwa kuwa katika dunia ya sasa michezo inatoa fursa ya ajira.

Alisema kuwa mchezo wa Gofu ni ajira tosha hivyo yuko tayari kujifunza mchezo huo wakati wowote na kuwaondoa hofu wanawake kwamba ni mchezo wa gharama.

Aliongeza kuwa kiwanja Bora cha gofu kiko kwenye wilaya ya Mufindi na serikali Iko tayari kuunga mkono mchezo huo kwa kuwa ni Moja ya chanzo Cha mapato kwa wilaya kwa kuwa wageni wengi wamekuja na kuingiza Hela maeneo haya.


Awali akisoma risala ya mashindano hayo kwa mgeni rasmi, Mmoja ya washiriki wa mashindano hayo , Yona Mbadime alisema kuwa mashindano yamekuwa na mafanikio makubwa  na kuweza kushirikisha wanamichezo takriban 44 ambapo Wanawake walioshiriki ni 4 kutoka kwenye vilabu vitano vya Lugalo Gofu, Kilombero , Gymkhana, Moshi na Mufindi.

Naye mwakilishi kutoka kampuni ya Asas, Mohamed Salim ambaye ni afisa masoko alisema kuwa kampuni hiyo Iko tayari kushirikiana na wanamichezo wa mchezo huo na wasisite pindi wanapohitaji msaada 


Alisema kuwa mchezo huo unazidi kuwa kivutio kwani hauchagui rika katika kucheza hivyo watu wajitokeze kushiriki na kufanya uwe na Wachezaji wengi zaidi.

Katika mashindano hayo washindi walijinyakulia zawadi mbalimbali zikiwemo tv flat screen , friji na radio na fedha taslimu.


MSAJIRI AWAKUMBUSHA WANASIASA KUZINGATIA SHERIA

$
0
0

NA MWANDISHI WETU

 

VYAMA vya Siasa nchini, vimekumbushwa kuzingatia kanuni na sheria ambazo zimetungwa ili kuleta amani na utulivu na wakisisitizwa kutumia lugha ya stara.

 

Pia wanasiasa wamekumbushwa kuhakikisha wanazingatia sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia masuala ya siasa nchini ili kutoleta mpasukakatika jamii.

Hayo yamezungumzwa leo jijini Dar es Salaam na Jaji Francis Mutungi wakati wa ufunguzi wa kikao cha kujadili mwenendo wa siasa nchini ulioandaliwa na Baraza la Vyama  vya Siasa.

 

“Wakati mwingine wanasiasa mnafanya mikutano ya ndani ambapo maofisa wetu huwa hawapo jambo ambalo wakati mwingine linapelekea kutoa lugha ambazo si sahihi kitu ambacho ni hatari kwa maslahi ya nchi.

 

“Ofisi ya Msajili si Polisi hivyo kama kuna changamoto yoyote imejitokeza katika shughuli zenu mnakaribishwa wakati wowote kwani tunajenga nyumba moja hakuna haja ya kunyang’ana fito,” amesema.

 

Pia naye Mwanasiasa mkongwe, John Cheyo amesema kuwa kikao hicho nia yake ni kujenga uhusuano mzuri kwa watanzania ambao siku zote wanahitaji amani na utulivu.

 

“Nimekua kwenye siasa kwa kipndi kirefu na nimezunguka katika mataifa mbalimbali na sikuona mwanasisasa aizungumzie vibaya nchi yake lakini kwa sasa nashuhudia baadhi ya wanasiasa hapa nchini wakiizungumzia vibaya nchi yetu nje ya mipaka ya Tanzania, tunakwenda wapi?, amehoji.

 

Naye Padri, Florence Rutaiwa ambaye ni Mkurugenzi wa Kurugenzi Kichungaji kutoka Baraza wa Wachungaji, amesema wao wakiwa ni sehemu ya viongozi wa dini kazi yao kubwa kushauri wanasiasa kufanya siasa za kistaarabu zinazompendeza Mungu.

 

Hivyo wakati wowote wanapoona wanasiasa wanakengeuka watawaona kupitia kwenye nyumba zao za ibada ili wafanye siasa safi kwa ajili aya kulinda amani ya nchi na si kupanda majukaani.

 

Viongozi wa dini kazi yetu ni kuhakikisha tunakemea dhambi kwa yeyote anayekengeuka katika majukumu yake ya kisiasa bila kumuonea mtu, amesema.

 

  Kwa upande wake, Amiri Mkuu wa Baraza Kuu na Jumuia za Taasisi za Kiislamu Tanzania Mussa Kundecha, amesema kwamba wakati mwingine ni vigumu kutofautisha shughuli za kisiasa na masuala ya dini kutokana na kwamba yote yanahusiana na usimamizi na mambo ya kijamii.

 

Hivyo mwanasiasa naye anajihusisha na mambo ya kijamii ingawa Siasa ina vigawo vingi, hivyo kiongozi wa dini si vema kujihusisha na siasa kutokana na kwamba inawezekana waumini wake wapo katika makundi tofauti ya vyama hivyo akijiingiza anaweza kuwaganya na kuleta machafuko.

 

Pia alibanisha kuwa dhambi ya kisiasa ni kubwa sana kwa maana inaweza kuathiri watu wengi kutokana na kwamba mtu anayetaka uongozi anaweza kuua watu wengi ili apate uongozi, hivyo inastahiri kukemewa kwa nguvu kubwa.


MASHINDANO YA MBUNGE CUP YAFIKIA PATAMU

$
0
0

 

Na John Marwa


Mashindano ya Mbunge Cup Jimbo la Ukonga maarufu kama Nane Nane Cup yamefikia patamu baada ya kupata timu za robo fainali ngazi ya vijana.


Hatua hiyo imefikiwa mara baada ya michezo iliyopigwa leo katika viwanja mbalimbali jimboni humo jioni ya leo.



Timu ya Naweza Youth imeifulusha mabao (3 - 0) Jagwa FC, Chanika City nao wametinga Robo Fainali kwa kuwaondosha kwa mikwaju ya penati (4-3) dhidi ya Wala Mboga FC,  Majohe United dhidi ya Kipunguni (hawakufika Uwanjani sababu ya msiba).


Wakati Chakenge wamitungua mabao (4-2) Msongola, Buyuni United wamewatupa nje Pugu United kwa mikwaju (5-4), Goms United wao wamefungisha virago vyao kwa penati (3-4) dhidi ya Pugu Stesheni.


Washindi wa michezo hiyo hapo juu wametinga Robo Fainali ya Jerry Silaa, Mbunge Cup ama Nane Nane Cup 2023 Jimbo la Ukonga ambapo hatua hiyo itapigwa Agosti 8 na kuaptikana washindi wa michezo hiyo na michezo mingine inayofanyika katika Bonanza hilo.

Francis Kiwanga; Teknolojia kuongeza kasi ya maendeleo

$
0
0

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation For Civil Society (FCS) Francis Kiwanga, akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Wiki ya Azaki iliyofanyika Agosti 1, 2023, Jijini Dar es Salaam.(Picha na FCS).

Mratibu wa Wiki ya AZAKi 2023, Justice Rutenge akizungumza katika hafla hiyo kuelezea namna kaulimbiu ya mwaka huu ilivyobeba dhima nzima ya Wiki ya Azaki.


 Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation For Civil Society (FCS) Francis Kiwanga, (wa pili kushoto), akiwa na Mbunge wa Kigamboni Dkt. Faustini Ndugulile pamoja na wadau wengine wakipiga makofi mara baada ya kufanyika kwa uzinduzi rasmi wa Wiki ya Azaki iliyozinduliwa Agosti 1,2023 Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa (FCS), Francis Kiwanga, (wanne kushoto), akiwa na Mbunge wa Kigamboni Dkt. Faustine Ndugulile (wa tano kushoto), pamoja na wadau wengine katika picha ya pamoja katika hafla hiyo.
 

 Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam


Mkurugenzi wa Foundation For Civil Society (FCS) Francis Kiwanga, amesema kuwa Teknolojia inaweza kuwa chachu ya kuongeza kasi ya maendeleo pamoja na kuwawezesha watanzania kuongeza uzalishaji, kutafuta masoko na hatimaye kukuza vipato vyao.

Kiwanga ameyasema hayo wakati wa uzinduzi rasmi wa Wiki ya Azaki iliyofanyika Agosti 1, 2023 Jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa lengo la kuwepo kwa Wiki ya Azaki ni kutazama kwa jinsi gani maendeleo ya teknolojia yanavyoweza kuwawezesha watanzania kuongeza uzalishaji, kutafuta masoko na hatimaye kukuza vipato vyao.

Aidha ameeleza kuwa mwaka 2018 Wiki ya Azaki ilifanyika kwa mara ya kwanza ambapo pamoja na mambo mengine walijifunza namna ya kuimarisha mahusiano yao na Serikali.

“Mnamo mwaka 2018 tulikutana kwa mara ya kwanza kwa ajili ya CSO Week, tulianza kujiuliza tunawezaje kuimarisha mahusiano yetu na Serikali.

“Lengo jingine lilikuwa ni kuwajengea uwezo (Capacity Building) kwa wananchi wa kawaida, ili kuweza kuboresha maisha yao, na kuleta tija katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo wananzozifanya” ameeleza Kiwanga.

Pia ameongeza kuwa, kufanyika kwa Wiki ya Azaki mwaka huu kutakuwa ni mwendelezo ikiwa ni mara ya tano kuzindua ikiwa ni  kuelekea kwenye Wiki ya Azaki itakayofanyika mwezi Ogasti 2023, lengo likiwa ni kuwagusa wananchi wanaowapa nguvu ya kufanyakazi kila siku.

“Mimi Binafsi kwa mfano, ninapata nguvu ya kufanya kazi kila ninapoona picha ya mama mmoja toka kijijini, akiwa na furaha na tabasamu kubwa baada ya kupata mavuno yake, hawa ndio wanaotupa msukumo wa kuendelea kufanya kazi na kufanya CSO Week kila mwaka” ameongeza Kiwanga.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), wakili Anna Henga, ameweka wazi kuwa moja ya haki za msingi za binadamu ni kufikia huduma za teknolojia ambapo amebainisha kuwa ukuaji wa Sayansi na Teknolojia utawezesha wananchi kupata taarifa mbalimbali kuhusiana na haki zao kupitia vifaa vya teknolojia.

Wiki ya Azaki inaleta pamoja Asasi za Kiraia (AZAKI ) Pamoja kutoka Tanzania nzima kwa ajili ya tukio la wiki moja lenye lengo la kujadili na kuboresha ushirikiano wa kimkakati ikiwa na Kauli mbiu isemayo ‘ Teknologia na Jamii . Tulipotoka, tuilipo sasa na tunapoelekea , kuangazia fursa na changamoto zinazotokana na ulimwengu wa teknolojia unaoendelea’

Mratibu wa Wiki ya AZAKi 2023, Justice Rutenge ameelezea kuhusu uchaguzi wa kaulimbiu ya mwaka huu iliyobeba dhima nzima ya Wiki ya Azaki ambapo amesema kuwa uchaguzi ulifanywa kwa madhumuni, na inalenga kuziwezesha asasi za kiraia kufahamu na kupata utaalamu unaohitajika ili kuishauri Serikali na Sekta Binafsi juu ya faida na vikwazo vinavyotokana na teknolojia kwa maendeleo ya nchi.

Wiki ya Azaki inatajiwa kuanza rasmi tarehe 23 hadi 27 Oktoba 2023 Jijini Arusha, ambayo inatokana na mafanikio ya matoleo yake ya awali ya mwaka 2018, 2019, 2021 na 2022, ambapo kwa mwaka huu inatarajiwa kuwa chachu ya mabadiliko, kukuza uelewa wa kina wa athari za teknolojia kwa jamii na nafasi yake inayowezekana katika kuunda.

WABUNIFU COSTECH WAMVUTIA MAKAMU WA RAIS DK MPANGO

$
0
0

 NA MWANDISHI WETU, MBEYA

MAKAMU wa Rais Dk. Philip Mpango, amekiri kuvutiwa na uwezeshaji kwa wabunifu wazawa unaofanywa na Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), aliyoitaka kuhakikisha inaenda mbali zaidi kwa kukifanyia kazi kilio chao cha kutaka kuwapatia Mafunzo ya Mifumo ya Kielektroniki, Ili kuwaongezea ufanisi katika bunifu zao.

Dk. Mpango ameyasema hayo Jumanne ya Agosti 1, alipotembelea Banda la COSTECH, wakati wa uzinduzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nane Nane (Tanzania International Agricultural Trade Show 2023), kwenye Viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya, ambako alikuwa mgeni rasmi na kuyazindua kwa kuitaka Wizara na mamlaka husika kutoa tuzo na zawadi za fedha kwa wabunifu wazawa

Akiwa COSTECH, Dk Mpango alivutiwa zaidi na mbunifu Adam Kinyekile 'Street Engineer,' aliyewezeshwa na tume hiyo kubuni Mashine Maalum ya kuchakata mazao, ikiwemo kupukuchua nafaka, kusaga nafaka zisizo na mafuta, kuvuta maji ya kumwagilia mazao na kuyabeba mazao hayo baada ya kuvunwa mashambani kupeleka ghalani, ambapo alipokuwa akitoa hotuba ya jumla ya uzinduzi rasmi mbele ya wahudhuriaji, alirudia kuimwagia sifa COSTECH, kwa uwezeshaji kwa kijana huyo na wenzake.

Dk. Mpango aliipongeza COSTECH kwa kuthamini bunifu za vijana wa Kitanzania, ambako alishuhudia bandani hapo bidhaa za Kilimo, Ufugaji na Ufundi kutoka kwa vijana walioshiriki Mafunzo Atamizi, kisha akasikiliza kero na changamoto zao na kuahidi kuzifanyia kazi, huku akiitaka tume hiyo kuwaongezea vijana wabunifu Mafunzo ya Kielektroniki, kama alivyoomba Kinyekile Ili kuongeza ufanisi wa bunifu zao, kwani liko ndani ya uwezo wao.

Akizungumzia ubunifu wa Mashine hiyo, Dk. Mpango alimpongeza Adam kwa ubunifu huo, lakini akamshauri kutenganisha kazi za mashine zitokanazo na ubunifu wake Ili kupunguza gharama yake ambayo inaweza kuwa ghali kwa mkulima wa kawaida kuimudu na kubainisha kuwa itakapotenganishwa na kila moja ikafanya kazi tofauti, zitashuka bei na kuwapunguzia mzigo wakulima.

"Kwanza nikupongeze kwa ubunifu huu, tunahitaji vijana wa Kitanzania wabunifu kama wewe. Nitumie fursa hii kuwaomba vijana wote wabunifu wenye uwezo wa kutengeneza Mashine za kuchakata mazao kama hizi wafanye hivyo, COSTECH ipo hapa kwa ajili ya kuwasaidia kama walivyokusaidia wewe na vijana wenzako.

"Mamilioni uliyopewa na COSTECH ni mengi, sio haba kwa mkulima kuyamudu, kwahiyo nashauri utenganishe mashine hizi Ili kupunguza gharama kwa mnunuzi ambaye ni mkulima," alisema Dk. Mpango na kuitaka tume hiyo kuwasaidia wabunifu hao Ili kubuni mashine tofauti tofauti zinazotumia Mifumo ya Kielektroniki kama alivyoomba Adam.

Awali, Afisa Uratibu na Utafiti wa COSTECH, Dk. Deogracious Protas, alimueleza Makamu wa Rais kuwa, licha ya Sh. Mil. 99 walizotoa kwa Adam, tume yake imesaidia Mafunzo Atamizi ya vijana wanaojihusisha na Kilimo, Uvuvi na Ufugaji, sambamba na kutoa mitambo yenye thamani ya Sh. Mil. 400 kuboresha usindikaji kwa Kituo cha Utafiti cha TARI Makutupola kilicho chini ya JKT Makutupola, ambayo imekuwa msaada mkubwa kwa wakulima wa zabibu inayosindikwa hapo kuzalisha mvinyo bora.

Dk. Protas alimuahidi Makamu wa Rais kuwa tume yake italifanyia kazi agizo lake la kutaka iwasaidie wabunifu wazawa kupata Mafunzo ya Kielektroniki Ili kuwawezesha kubuni kwa faida bidhaa zenye mifumo hiyo kwa ustawi wa wakulima na Sekta ya Kilimo, Uvuvi na Ufugaji kwa ujumla, Ili iweze kutoa mchango kwa ukuaji wa uchumi wa nchi na kuongeza mchango wa Sekta hiyo katika kukuza Pato la Taifa.

Makamu wa Rais Dk Philip Mpango(katikati) akikata utepe wakati wa uzinduzi wa maonyesho ya Kimataifa ya Kilimo Nanenane jijini Mbeya
Makamu wa Rais akipata maelezo kutoka kwa Afisa uratibu na utafiti wa COSTECH, Dk Deogracious Protas wakati alipotembelea Banda kwenye maonyesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa jijini Mbeya . Kulia Mbunifu wa Mashine ya kuchakata mazao. Adam Kinyekile.
 Makamu wa Rais, Dk Philp Mpango akimsikiliza Mtafiti wa Mifugo,Mark Mark wakati akitoa maelezo ya Dawa mbalimbali alipotembelea Banda la Tume ya Sayansi na Teknolojia COSTECH kwenye maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya.NA MWANDISHI WETU, MBEYA

MAKAMU wa Rais Dk. Philip Mpango, amekiri kuvutiwa na uwezeshaji kwa wabunifu wazawa unaofanywa na Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), aliyoitaka kuhakikisha inaenda mbali zaidi kwa kukifanyia kazi kilio chao cha kutaka kuwapatia Mafunzo ya Mifumo ya Kielektroniki, Ili kuwaongezea ufanisi katika bunifu zao.

Dk. Mpango ameyasema hayo Jumanne ya Agosti 1, alipotembelea Banda la COSTECH, wakati wa uzinduzi wa Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nane Nane (Tanzania International Agricultural Trade Show 2023), kwenye Viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya, ambako alikuwa mgeni rasmi na kuyazindua kwa kuitaka Wizara na mamlaka husika kutoa tuzo na zawadi za fedha kwa wabunifu wazawa

Akiwa COSTECH, Dk Mpango alivutiwa zaidi na mbunifu Adam Kinyekile 'Street Engineer,' aliyewezeshwa na tume hiyo kubuni Mashine Maalum ya kuchakata mazao, ikiwemo kupukuchua nafaka, kusaga nafaka zisizo na mafuta, kuvuta maji ya kumwagilia mazao na kuyabeba mazao hayo baada ya kuvunwa mashambani kupeleka ghalani, ambapo alipokuwa akitoa hotuba ya jumla ya uzinduzi rasmi mbele ya wahudhuriaji, alirudia kuimwagia sifa COSTECH, kwa uwezeshaji kwa kijana huyo na wenzake.

Dk. Mpango aliipongeza COSTECH kwa kuthamini bunifu za vijana wa Kitanzania, ambako alishuhudia bandani hapo bidhaa za Kilimo, Ufugaji na Ufundi kutoka kwa vijana walioshiriki Mafunzo Atamizi, kisha akasikiliza kero na changamoto zao na kuahidi kuzifanyia kazi, huku akiitaka tume hiyo kuwaongezea vijana wabunifu Mafunzo ya Kielektroniki, kama alivyoomba Kinyekile Ili kuongeza ufanisi wa bunifu zao, kwani liko ndani ya uwezo wao.

Akizungumzia ubunifu wa Mashine hiyo, Dk. Mpango alimpongeza Adam kwa ubunifu huo, lakini akamshauri kutenganisha kazi za mashine zitokanazo na ubunifu wake Ili kupunguza gharama yake ambayo inaweza kuwa ghali kwa mkulima wa kawaida kuimudu na kubainisha kuwa itakapotenganishwa na kila moja ikafanya kazi tofauti, zitashuka bei na kuwapunguzia mzigo wakulima.

"Kwanza nikupongeze kwa ubunifu huu, tunahitaji vijana wa Kitanzania wabunifu kama wewe. Nitumie fursa hii kuwaomba vijana wote wabunifu wenye uwezo wa kutengeneza Mashine za kuchakata mazao kama hizi wafanye hivyo, COSTECH ipo hapa kwa ajili ya kuwasaidia kama walivyokusaidia wewe na vijana wenzako.

"Mamilioni uliyopewa na COSTECH ni mengi, sio haba kwa mkulima kuyamudu, kwahiyo nashauri utenganishe mashine hizi Ili kupunguza gharama kwa mnunuzi ambaye ni mkulima," alisema Dk. Mpango na kuitaka tume hiyo kuwasaidia wabunifu hao Ili kubuni mashine tofauti tofauti zinazotumia Mifumo ya Kielektroniki kama alivyoomba Adam.

Awali, Afisa Uratibu na Utafiti wa COSTECH, Dk. Deogracious Protas, alimueleza Makamu wa Rais kuwa, licha ya Sh. Mil. 99 walizotoa kwa Adam, tume yake imesaidia Mafunzo Atamizi ya vijana wanaojihusisha na Kilimo, Uvuvi na Ufugaji, sambamba na kutoa mitambo yenye thamani ya Sh. Mil. 400 kuboresha usindikaji kwa Kituo cha Utafiti cha TARI Makutupola kilicho chini ya JKT Makutupola, ambayo imekuwa msaada mkubwa kwa wakulima wa zabibu inayosindikwa hapo kuzalisha mvinyo bora.

Dk. Protas alimuahidi Makamu wa Rais kuwa tume yake italifanyia kazi agizo lake la kutaka iwasaidie wabunifu wazawa kupata Mafunzo ya Kielektroniki Ili kuwawezesha kubuni kwa faida bidhaa zenye mifumo hiyo kwa ustawi wa wakulima na Sekta ya Kilimo, Uvuvi na Ufugaji kwa ujumla, Ili iweze kutoa mchango kwa ukuaji wa uchumi wa nchi na kuongeza mchango wa Sekta hiyo katika kukuza Pato la Taifa.

Makamu wa Rais Dk Philip Mpango(katikati) akikata utepe wakati wa uzinduzi wa maonyesho ya Kimataifa ya Kilimo Nanenane jijini Mbeya
Makamu wa Rais akipata maelezo kutoka kwa Afisa uratibu na utafiti wa COSTECH, Dk Deogracious Protas wakati alipotembelea Banda kwenye maonyesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa jijini Mbeya . Kulia Mbunifu wa Mashine ya kuchakata mazao. Adam Kinyekile.
 Makamu wa Rais, Dk Philp Mpango akimsikiliza Mtafiti wa Mifugo,Mark Mark wakati akitoa maelezo ya Dawa mbalimbali alipotembelea Banda la Tume ya Sayansi na Teknolojia COSTECH kwenye maonesho ya Nanenane yanayofanyika katika viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya.

NEC YASHIRIKI MAONESHO YA KILIMO NANE NANE KANDA YA KATI

$
0
0
TUME ya Taifa ya Uchaguzi nimongoni mwa taasisi mbalimbali za binafsi na serikali zinazoshiriki katika Maonesho ya Wakulima maarufu kama Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma na kuwapa fursa wananchi hasa wakazi wa mikoa ya Kanda ya Kati kupata elimu ya Mpiga Kura ambayo hutolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
 
Katika banda la NEC wananchi mbalimbali wameweza kutembelea leo Agosti 1,2023 ikiwa ni siku ya kwanza ya maonesho hayo ya siku 10.
 
Wananchi hao waliweza kuuliza maswali mbalimbali ambayo yalipatiwa majibu kutoka kwa maofisa wa Tume. 
 
Wananchi waliotembelea banda la Tume, wakiangalia Album iliyo na picha za uteuzi wa wagombea katika Uchaguzi Mkuu wa 2020.
Afisa wa NEC, Nuru Riwa akitoa amelezo kw mgeni aliyefika katika Banda la Tume.
Afisa wa NEC, Loshilu Saning'o akitoa amelezo juu ya matumizi ya BVR inavyo  fanya kazi wakati wa uboreshaji.
Maofisa wa Tume wakitoa Elimu ya Mpiga Kura kwa wageni waliofika Bandani.
Maofisa wa Tume wakitoa Elimu ya Mpiga Kura kwa wageni waliofika Bandani.

JKT LAHIMIZA WANANCHI WA MKOA WA MBEYA KUFIKA KWENYE BANDA LAO KUJIFUNZA SHUGHULI ZA KILIMO

$
0
0

Na Richard Mrusha, Mbeya

JESHI la kujenga Taifa Nchini(JKT) limewataka wananchi wa Mkoa wa Mbeya na Mikoa jirani kuendelea kujitokeza kwa wingi kwenye banda lake lililopo katika viwanja vya John Mwakangale ambako maonesho ya nane nane yanaendelea na kwamba wafike ili kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu shughuli za kilimo na kuongeza kuwa kwa upande wa shuguli zinazofanywa na jeshi hilo, ikiwa ni shirika la uzalishaji mali la Suma JKT pamoja na vikosi, shule na chuo.



Pia jeshi hilo limesema kuwa mbali na kutoa mafunzo katika nyanja za kilimo, mifugo na uvuvi lakini vilevile linatoa elimu kwa watanzania wote kuhusu sekta ya kilimo pamoja na mambo mengine.

Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa majeshi Nchini, pamoja na mkuu wa jeshi la kujenga Taifa,Mkuu wa Tawi la Utawala Jeshi la kujenga Taifa Buligedia Hassan Rashid Mabena ameyasema hayo Jijini Mbeya Agost 1,2023 baada ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philp Mpango kuzindua maonesho hayo.

Kufuatia hali hiyo buligedia Mabena ametumia nafasi hiyo kuwaasa wananchi hao kufika kwenye banda la JKT ambapo watajionea shughuli za kilimo ambazo zinafanywa, na jeshi la kujenga Taifa lenyewe linajihusisha na uzalishaji wa mazao ya chakula yakiwemo mazao ya mahindi, mpunga, Maharage pamoja na alizeti.

Alisema kuwa mazao mengine yanayozalishwa na jeshi hilo ni pamoja na mazao ya mbogamboga ambazo zinapatikana kwa wingi katika bustani zao lakini pia mazao ya biashara ya kimkakati kama zao la kahawa, chikichi, korosho pamoja na mkonge.

''Wananchi wafike hapa banda la JKt ili kujionea shughuli za kilimo zinazofanywa na jeshi hili lakini pia shughuli za ufugaji na uvuvi, jeshi la kujenga Taifa linajihusisha ufugaji wa mifugo ikiwa ng'ombe, mbuzi, kuku, lakini vilevile na ufugaji wa samaki lakini tunatoa elimu ya ufugaji wa samaki na nirahisi sana ambapo hata mfugaji ana eneo dogo sana na akaweza kuweza kufuga kisasa na akaweza kujipatia kitoweo lakini vilevile kuweza kujipatia mapato kuuza wale samaki ambao atawazalisha katika eneo lake dogo kwahiyo niwaase waje kwa wingi na kuweza kupata mafunzo hayo,''alisema Buligedia Mabena.

Aliongeza mafunzo hayo yanatolewa kwa vijana kupitia wataalamu wa kilimo wa jeshi hilo na kubainisha kuwa mafunzo yanatolewa kwa kundi la vijana wa lazima kwa maana ya mujibu wa sheria na lile kundi la vijana wa kujitolea.


Viewing all 19659 articles
Browse latest View live